Friday, July 16, 2010

KUMBE KRE-GALS HALISI HAWA KWEPO KWENYE VIDEO YA TEACHER.

siku ya jana (alkhamis ) kabla ya bongela show walio tupia pale NGOME KONGWE KRE-GALS wali weza kudondoka kwenye mjengo wa Hits fm radio hapa zanzibar.

wakiwa na prodyuza wao LAMAR na msani mwenzao YOUNG DEE. kitu ambacho walizungumzia ni kuwa hawakupata nafasi ya kushiriki kwenye video ya wimbo wa Young Dee  "TEACHER" kwa sababu walikua busy na skonga..so watu wengi wakafikiria kuwa wale kwenye video ya teacher ndio kre-gals,kumbe sio. so siku ya jana wali weka wazi hilo na kulitolea ufafanuzi kiundani zaidi.

kikali zaidi ni kwamba kuna pini jipya ambalo waliweza kulitambulisha ndani ya kipindi cha "POWER ENTERTAINMENT RELOADED"

KRE-GALS wanatambulika  kwa majina yao mengine ambao  mmoja wao ni "TATA" na mwengine ni "YOYO"  na jina la ngoma yao mpya ni "SITARUDIA"ambao wameshirikiana na mkali wa  michano Binamu a.k.a Mwana F.A..lakini pia Young Dee, alituachia mzigo wake mpya...hayo yote ndio mambo ya FISH CRAB !!!

No comments:

Post a Comment