Thursday, July 29, 2010

CHAMELEONE AMPA KICHAPO MDOGO WAKE MAURICE KIRYA" VAMPINO "......

Watu wengi wamezungumza..juu ya kitendo cha mwanamuziki jose chameleone kumpiga msani mwenzake tokea nchini uganda aitwae VAMPINO .hayo yote yalifanyika siku ya j5 nje ya club silk ...kiwanja maarufu nchini humo cha muziki.inasemekana kuwa chanzo ni kwaNINI Vampino hamkubali jama..kwa hiyo ye chameleone anaona  kama jama anamdharau.wengi wanasema kuwa huyu jama (chameleone) tabia yake sio nzuri..tangu apate fursa ya kuonyesha sanaa yake kwenye jukwa wa la kombe la dunia..
Vampino alilazwa hospitali kansanga na watu wake wamefungua kesi dhidhi ya jose chameleone katika kituo cha police  jinja road...

badhi ya watu tokea nchini humo wamesema haya kupitia mtandao wa urafiki facebook..

kaka yake Vampino bwana Maurice kirya ambae pia ni msani kasema haya

"

I was blind but now i see, with blows to his face, he wondered why he
was attacked,and the answer was,because he did not worship the Dr.
Joseph chameleon! i hope my brother vamposs recovers from the injuries
and dis figured face, i love his music, but chameleon has attacked many,
and is protected by all of us. We have ..."


mtu mwengine ambae ni mtangazaji wa kituo cha redio hot 100 jijini kamapala kaesema haya
bwana 
"

Banange Chameleon...wateva they say u did to My boy Vampos was such a cheap shot. I love yo music bt smthangz take the love away."

Tuesday, July 27, 2010

MAPENZI NDANI YA BIG BROTHER TAYARI

Kulikuwa na habari kuwa Sheila kutoka nchini Kenya na Hanningtone kutoka uganda walikuwa na kiji issue flani cha mapenzi kilicho kuwa kinaendelea..Kwa kuweka mambo sawa Sheila alikata kabisa swagga hizi za kuwa ana feel lolote kwa chali huyo kutoka uganda na hapo baadae aliskika jama Hanningtone akiwa anamlalamikia kwanini alimvunja moyo...duh ! hii kali..na kwa habari nyingine ,siku ya jana (j3)Tatiana alitolewa (kwa maana ya kwamba she was voted out like eviction) kwenye jumba la B.B.A...lakini..akarudishwa tena..

NYOTA WA MUZIKI MWENYE ASILI NA CHIMBUKO YA NCHINI HAITI AMETANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAISI

wycleff jean anae ishi nchini marekani kwa sasa ,ametangaza nia ya kugombea cheo cha uraisi..nchini haiti..kwa saivi ni balozi wa Haiti nchini marekani lakini nia yake anasema ilianza mwaka 2007 wakati alivyo teuliwa kuwa balozi wa nchi Haiti...Japokuwa raisi aliopo madarakani kwa sasa Rene Preval hana nia ya kugombea tena,Wycleff kasema ye binafsi ataendelea kutoa misada kwa watu wake wa Haiti na kuwa karibu nao katika kipindi hichi kigumu walicho nacho kwa sasa....




LAURYN HILL NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

Msani wa kitambo alie tikisa sana ulimwengu wa mziki miaka ya tisini..Lauryn Hill alikua nchini Rwanda siku ya juma pili ambapo alitupi bongela show Katika tamasha la FESPAD..kama ilivyo kawaida walikwepo wakali wengine kama jose chameleone toka nchini uganda na pili pili toka nchini Kenya NA WENGINEO KIBAO..

Kilicho shangaza zaidi ni kwamba ame achia ngoma yake mpya(REPERCUSSIONS) nchini humo (KIGALI)hata kabla ya kuiachia marekani anapotokea mwana dada huyo..na pia miss Hill ata tupi performance kwenye tamasha lingine nchini marekani linalojulikana kama ROCK BELLS

Sunday, July 25, 2010

HII KALI..TUNAFAHAMISHWA KUWA JIGGA ANASAFIRI NA TOILET PAPER YAKE SPECIAL KILA SEHEMU AENDA KO

Mwana muziki toka kasabia Tom Meighan, ameeleza  kwanini hajahisi kama ye ni maarufu,miongoni ni kuwa ,hajapata toilet paper zake na choo kama jayz.jama vile vile anasema akibahatika kuwa na hivyo vitu hapo basi naye atajijua kama ni nyota na ni maarufu..


 .inasemekana kuwa Hov kila anapo safiri ku perform kwenye festival mbali mbali uwa ana burungutu la toilet paper na private toilet. HOV anasema kwenye mistari ya kinyamwezi kuwa ana shida 99..ila kumwabukiza wadudu wako sio moja ya shida hizo...


"

"I Got 99 Problems & Your Germs Aint One: Jay-Z Takes Private Toilet With Him Everywhere"

fiesta ipo home kwetu zanzibar....

MWENZETTU LUIS KOLUMBIA AKIUZURIA MKUTANO WA WAGOMBEA

Friday, July 23, 2010


VODACOM FOUNDATION KUDHAMINI GALA NIGHT ZANZIBAR


Meneja wa Mfuko wa Vodacom fondition, Yessaya Mwakifulefule 8kushoto na mbunifu wa mavazi Mstapha Hassanali wakizungumza na waandishi wa habari

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom kwa kushirikiana na mbunifu wa mavazi Mstapha Hassanali imejitokeza kudhamini maonesho ya mavazi ya hisani yanayolenga kuboresha hali ya mazingira ya Hospital ya wenye matatizo ya akili ZANZIBAR.

Maonesho hayo yanayofahamika kama 'Fashion 4 Health Black and Gold Gala' yanafanyika mara ya tatu mfururizo yanaandaliwa na Exprlore ZANZIBAR yatafanyika tarehe 30 Julai mwaka huu katika Hotel ya Serena Inn Mjini humo.

"Kwa kuthamini umhimu wa jamii ambayo tunafanya nayo kazi na kwa Heshma ya Maryam Olsen wa Explore Zanzibar tumeshawishika kudhamini onesho hili kuchangia majengo ya Hospitali hiyo," alisema Mwakifulefule.

Naye mbunifu maarufu wa mavazi nchini Mstafa Hassanali alisema katika maonesho hayo atazindua mtindo wake mpya wa mavazi unaofahamika kama 'KARAFUU Collections', akiambatana na wanamitindo wengine 10 kutoka Tanzania bara wakisindikizwa na burudani kutoka katika bendi ya Tanzanite.

Alisema mbunifu mwingine wa Mavazi Farouque Abdella wa zanzibar atafungua pazia la maonesho hayo akifuatiwa na mbunifu Mago ambapo wadhamini mbalimbali wakiwemo PSI Tanzania, 361 degree Events na Mstapha Hassanali Couture wamejitokeza kudhamini maonesho hayo.

"Wagonjwa wana kila sababu ya kujifunza na kuishi katika mazingira ya kupendeza lakini tunahitaji msaada na mimi kwa kushirikiana na wenzangu tutashiriki kikamilifu katika onesho hilo kuchangisha fedha," alisema hassanali.

UZINDUZI WA MSANI AT KUKUSANYA WASANI NYOTA TOKA TANZANIA NA KENYA

miongoni mwa wasani watakao kwepo ni, Shiko,Mheshimiwa temba, ali kiba, berry black, hussein machozi, baby j, doricah, jelly wa rhymes, black, k.r. kutoka   tmk, nyota ndogo kutoka mombasa...

Tuesday, July 20, 2010

MWISHO MWANA KUTOKA MO TOWN KAREJEA BIG BROTHER AFRICA

Chali ka'amua kurudi big brother kuonyesha ma skillz yake..alikwepo na afro mwanzoni lakini mara hii, amengia na kipara..so tayari amesha onyesha mabadiliko kati ka maisha yake..hehehehehe.. tumsubirie kwa sana tuone swagga za mara hii..

Friday, July 16, 2010

KUMBE KRE-GALS HALISI HAWA KWEPO KWENYE VIDEO YA TEACHER.

siku ya jana (alkhamis ) kabla ya bongela show walio tupia pale NGOME KONGWE KRE-GALS wali weza kudondoka kwenye mjengo wa Hits fm radio hapa zanzibar.

wakiwa na prodyuza wao LAMAR na msani mwenzao YOUNG DEE. kitu ambacho walizungumzia ni kuwa hawakupata nafasi ya kushiriki kwenye video ya wimbo wa Young Dee  "TEACHER" kwa sababu walikua busy na skonga..so watu wengi wakafikiria kuwa wale kwenye video ya teacher ndio kre-gals,kumbe sio. so siku ya jana wali weka wazi hilo na kulitolea ufafanuzi kiundani zaidi.

kikali zaidi ni kwamba kuna pini jipya ambalo waliweza kulitambulisha ndani ya kipindi cha "POWER ENTERTAINMENT RELOADED"

KRE-GALS wanatambulika  kwa majina yao mengine ambao  mmoja wao ni "TATA" na mwengine ni "YOYO"  na jina la ngoma yao mpya ni "SITARUDIA"ambao wameshirikiana na mkali wa  michano Binamu a.k.a Mwana F.A..lakini pia Young Dee, alituachia mzigo wake mpya...hayo yote ndio mambo ya FISH CRAB !!!

MR.BLUE AULIZA SWALI ,DIVA NDIO NANI..?

Siku za nyuma kidogo kwa wewe ambae ulikua haufahamu ni kwamba kuna mwana dada anaitwa Diva .habari zilianza kuvuma kuwa Blue anamsumbua .sasa kwa upande wake .Blue anasema mimi simjuhi huyo DIVA (mtangazaji wa kituo kimoja cha redio jijini dar-es-salaam)lakini kitu kinacho nishangaza ni kwamba, naskia habari zina vuma kati ka vyombo vya habari mbali mbali hapa nchini kuwa mimi BLUE ninamsumbua huyo DIVA .kitu cha kwanza hatujawahi kukutana mi na yeye. sasa watu wanavyoandika hizo habari sijuhi wanazitoa wapi.
Ni hayo tu ! kutoka kwa Blue a.k.a KABISA...ila kwa misemo ya siku hizi ni kwamba itafahamika tu !!
.

Thursday, July 15, 2010

MKALI WA CAKE ISIO OZA (ALBINO FLANI )NA MSANI WA KIKE PIPI WAMETUPIKIA KITU KIKALI

Mchizi huyu anae kwenda kwa jina la kimziki kama Albino fulani yupo unyamwezini (marekani) ambapo yupo based ki maisha na kazi.hili goma jipya waliotupikia na mwana dada PIPI mara hii linakwenda kwa jina USIHOFU .. la  Fulani yuko mbioni kutoa album ambayo mapato yake ataelekezea katika kusaidia Maalbino wenzake kama mchango na chachu ya kuamsha albino wenzake kuwa wasikate tamaa na maisha kwani nafasi bado wanayo kama alivyowaambia kwenye track yake iliyopita ambayo alimshirikisha MwanaFa, Belle9, & Sugu.


Hivi karibuni Albino Fulani alitoa misaada ya lotions za kinga za jua kwa maalbino wenzake Tanzania kupitia shirika lisilo la kiserikari la Afrobino.org katika jitihada zake za kupambana na Cancer ya ngozi.

hapokweli ndio unaona bidi ya mchiz.jama  yupo serious na anthamini kweli ndugu zake hawa.pamoja sana kaka umoja ni nguvu

marafiki zetu walio tutembelea ndani ya wiki mbili hizi...

Tuesday, July 13, 2010

HATIMAE PINGU ZA MAISHA ZAFUNGWA KATI KA MARTIN LAWRENCE NA MPENZI WKE WA MDA MREFU..

Jama alie jijengea umaruufu kwa kuigiza kama komedian hatimae ameamua amuoe mpenze wake wa mda mrefu..tukio hili limefanyika kisiri kama ilivyo siku zote kwa watu maarufu nchini marekani..ka sherehe haka kalikuwa ka waatu maaluum tu.

jama alifahamika sana kwa movie Zake alio i cheza na chizi mwenzake will smith. (BIG MOMMA'S HOUSE 1&2, BAD BOY 1 & 2) Lakini pia ana movie nyingine pia ambao ni nzuri sana, zikiwemo..THIN LINE BETWEEN LOVE AND HATE alio i cheza na mkongwe mwengine katika anga za filamu Angella Bessette,RASCOE JENKINS na nyingine kibao...

Saturday, July 10, 2010

CHAMELEONE NDANI YA SAUZ NA MKE WE .ATATUMBWIZA J-PILI SAA MOJA KAMILI JIONI

msani huyo toka nchini uganda amesha tua sauz akiwa na mke we Daniella .amekutana  na wasani mbali mbali toka hapa barani afrika,kama 2face,samini na wengine toka bara la marekani kama shakira .wasani hawa ni miongoni mwa wale ambao wanatakiwa kutupia bongela show la kufunga kombe la dunia nchini humo.

KULIA NI CHALI AKIWA NA WIFE WAKE DANIELLA..


HAPA MWANA NA WAKALI WENGINE
TOKA NCHI MBALI MBALI NDANI NA NJE YA AFRIKA AMBAO PIA WAPO KWA AJILI YA KUTUMBWIZA NDANI YA SOCCER CITY.
MAMBO YA KUOMBANA KUPIGA PICHA NAYO YALI KWEMO ..HAPO MKE MTU AKIPIGA PICHA NA SHAKIRA NA VILE VILE MME MTU NAYE AKIZUGA
LAKINI MPANGO WAKE PIA TULI UJUA . NAOMBA
 TUPIGE PICHA YA KUMBUKUMBU..

KUMBE MASTAR NAO WANA SWAGGA HIZO ZA KUTAKA WAPIGE PICHA NA MTU ALIE JUU YAKE
HEHEHEHEHEHEHEHE...!!!

Thursday, July 8, 2010

RECOVERY TAYARI IMETINGA PLATINUM

jama toka PANDE ZA Detroit nchini marekani almarufu kama EMINEM a.k.a Marshall mathers,tayari ameshafikisha mauzo ya PLATINUM manake mauzo ya cd zaidi ya millioni moja na laki moja (1,100,000)ya album yake mpya RECOVERY.album hii ilingia sokoni mda wa kama wiki mbili nyuma.lakini kitu ambacho kinawashangaza watu ni kwamba,hata kati ka soko gumu la siku hizi ambao mauzo ni YA ku hustle sana japo upate certified GOLD,(mauzo zaidi ya laki tano).jama ye anazidi kuchana mauzo ya platinum..kwa kumbu kumbu tuna kufahamisha ni kwamba eminem album zake zote zimegonga PLATINUM kasoro ile ya kwanza ya REAL SLIM SHADDY..
Na vile vile album yake mchiz ni kwamba inaongoza billboard top 200 albums kwa week ya pili mfululizo sasa..

KIDOGO JAYZ AMPOTEZE BEYONCE NCHINI UINGEREZA...

Habari zilizo tufikia kutoka  nchini uingereza kupitia gazette la the SUN zinasema kua mwana dada Beyonce ,alikoswa kugongwa na taxi nchini uingereza siku ya jana (juma tano)mara baada ya kufungua mlango ili aweze kutoka kwenye gari,ila kilicho msisimua ni kwamba alivyo fungua tuu , mlango alishangaa tuu mlango kuondoshwa na gari nyengine. tukio hili lilitokea wakati ndio wanataka washuke  kwenye gari aina ya mercedes benz yenye rangi ya silver ambao walikuwa wakisafiria yeye na mme we JAY-Z.
washkaji walikua wanaelekea  kufanya shopping then ndio waeleke kwenye dinner eneo liitwalo swanky London eatery, Zuma, in Knightsbridge..lakini mara baada ya tukio hili ni kwamba, Beyonce alishtuka sana na shopping haikuendelea wala nini..dah !!! mASKINI...!!! inamaana JAYZ angebaki bila bila ???  wheeeewwwwwwwww...!!! balaa..

Wednesday, July 7, 2010

GEORGE MICHAEL ALIPATA AJALI TENA SIKU YA JUMA PILI...

msani huyo mwenye umri wa miaka 47,alikamatwa majira ya kuamkia siku ya juma pili saa tisa na nusu (3:35 am) polisi wa mji wa london walipigiwa simu na watu wanao kaa eneo hilo.baada kupokea simu kwa faster polisi wali ibuka eneo hilo la ajali papo kwa hapo. japo kuwa jama alipata ajali,alishtakiwa na kwa kosa la kuendesha gari nchini  akiwa anasadikika kuwa kalewa.

msani huyo bwana GEORGE, miaka 3 ya nyuma nazungumzia mwaka wa 2007 alikatazwa kuedesha gari kwa miaka 2,mara baada ya kugonga maduka ya kusafishia picha yaliopo karibu na nyumbani kwake maeneo la leafy kaskazini mwa mji wa London.

jama katoka kwa kulipa bondi ya kiasi cha fedha ambacho hakija wekwa wazi,lakini case hiyo itaendelea mwezi wa nane mwaka huu...

Tuesday, July 6, 2010

MWANA MUZIKI DMX AMEACHIWA UHURU LEO TOKA GEREZA LA ARIZONA

X mwenye majina halisi Earl Simmons, aliwekwa ndani mwanzoni mwa mwaka huu mara baada ku vunja sharti ya probation yAKE kwa kutumia madawa ya kulevya tena. lakini asubuhi ya leo mkali huyo wa muziki wa hip hop ameachiwa uhuru toka gereza hilo.kwa kukumbusha ni kwamba ni gereza hili hilo ambao limetoa probation ya miaka 3 kwa mwana muziki mwengine nchini marekani anaetambulika kwa jina la LIL WAYNE a.k.a DWAYNE CARTER..wayne ata anza kifungo cha nje mara baada kutoka gereza la Rikers island jijini Newyork .

Thursday, July 1, 2010

MB-DOGG NDANI YA UK...LAKINI, TATIZO..PLAY BACK CD....!!!

msani MB-DOGG yupo nchini uingereza kwa ajili ya kupiga show kali nchini humo.lakini kwa upande wangu, kuna kitu kimoja ambacho kimenitatiza.nimebahati kakuona badhi ya picha toka kwenye concert ambao Doggy katupia pale mji wa milton keynes ..

PROMOTER WAPI LIVE BAND..NA NI KWANINI PLAYBACK ?????
Hapa sijajua kwamba msala nimtupie nani !!!!..tuanzie kwa huyu mletaji msani .promoter unamleta msani toka afrika alafu anaimba juu ya cd(playback) hapo lengo hasa la kumleta huyo msanii kwa wale mashabiki wake ni lipi...? kama anaimba na cd..mie nilikuwa nafikiria kuwa ma promoter jaribuni kuwa sistizia wasani ambao mna wapeni mashavu ya kwenda nje kutangaza sanaa yao..waiimbe kupitia live band sio mambo ya play back cd..hapo tutakuwa tunainua na kukuza vipaji na vile vile kunenepesha mifuko ya wasani hao..coz ..naona wasani wanao imba live music mashabiki wao wana furahi na vile vile kuwaleta wasani kama wale ni gharama coz wanatoa burudani halisi sio cd play back..lakini mkaka DOGGY hongera but step up the Game to live band music kaka ..hicho ndio kitu ambacho dunia inataka kutokwa kwa wasani halisi sio wababaishaji..

BARUA YA SUGU KWA WANAINCHI



KATIKA KA BARUA YAKE SUGU Anasema HIVI.......................napenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha wananchi wenzangu wa Mbeya Mjini, wapenzi wa muziki wangu, wanachama wenzangu wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla tarehe 28 Juni 2010 nilikamatwa na polisi kwa kile walichonieleza kuwa kuna malalamiko dhidi yangu kuwa nimemtishia kwa maneno kumuua Ruge Mutahaba kupitia wimbo uitwao “Wanna Kill” uliopo kwenye album iitwayo “Anti Virus”.

Walinikamata saa 5 asubuhi nikiwa naingia ukumbi wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa ajili ya kutoa Mada kuhusu “Tathmini ya Muziki wa Kizazi Kipya na Hatma yake nchini” na kunihoji kwa takrabani masaa matano mpaka saa 10 jioni.

Wameniachia kwa kile walichonieleza kuwa ‘dhamana ya kujidhamini mwenyewe’ na kunitaka niripoti kwao siku ya jumatano tarehe 30 Juni saa 5 asubuhi siku ambayo nilipanga kwenye ratiba zangu kurejea nyumbani Mbeya Mjini kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kabla ya tarehe ya mwisho ya utoaji na upokeaji fomu ndani ya CHADEMA.

Katika mahojiano nao yaliyofanyika Makao Makuu ya Upelelezi Wizara ya Mambo ya Ndani; maofisa usalama (CID) walionihoji walirejea mstari mmoja katika kiitikio cha wimbo husika wenye maneno “I Wanna Kill Right Now” na kusema kwamba mlalamikaji ameutafsiri mstari huo kuwa ni tishio la kutaka kumuua.
Napenda kuwajulisha mashabiki wangu na watanzania wenzangu kwamba nimelieza wazi jeshi la polisi kwamba hakuna wimbo wala maneno niliyowahi kutamka kwa lengo la kukusudia kumuua binadamu yoyote. Niliwaeleza jeshi la polisi kwamba sanaa ya muziki inalugha zake zake za kifasihi.

Maadhui ya wimbo mzima yamejikita katika harakati zangu za siku zote za kupambana na wanyonyaji dhidi ya maslahi ya wasanii Tanzania na wimbo huo una maudhui ya kutaka “Kuondoa ama kuiua dhamira ya mbovu na nia zao ovu”.

Ni vyema mashabaki wangu, wanachama wenzangu na watanzania kwa ujumla wakarejea katika Kamusi mbalimbali za kimataifa ambapoo neno KILL linamaana zaidi ya 10 zikibeba pia maana ya KUKOMESHA, KUONDOA nk.

Katika wimbo huo nimeghani kwa kutumia fasihi mambo ya ukweli yanayotokea katika sekta ya sanaa na wala hauna dhamira yoyote wala maudhui ya kufanya kosa lolote la jinai; hivyo kama kuna mtu ameguswa na ukweli uliomo katika wimbo huo na hakubaliani nao basi aupinge kwa hoja ama akafungue madai badala ya kukimbilia kutaka kuliingiza jeshi la polisi kwenye masuala ya sanaa.

Aidha nimeshangazwa na hatua ya jalada hilo la polisi kufunguliwa ndani ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Wizara ya Mambo ya Ndani yaliyopo Wilaya ya Ilala wakati mimi na mlalamikaji wote ni wakazi wa Wilaya ya Kinondoni.

Baada ya maelezo niliyoyatoa ni matumaini yangu kuwa jeshi la Polisi ambalo lina kazi muhimu zaidi ya kukabiliana na ujambazi na vitendo vingine vya uhalifu ambavyo vinazidi kuongezeka katika Mkoa wa Dar es salaam ambapo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi yapo litaelekeza nguvu zake katika kukabiliana na vitendo hivyo vya makosa ya Jinai badala ya kupoteza muda wake kushughulikia masuala ya kifasihi ambayo yana sura ya madai yasiyo na uzito wowote.
Lakini vile vile Kwa sasa Mheshimiwa mtarajiwa yuko Mkoani Mbeya akiwa kwenye mchakato wa kurudisha fomu baada ya kupata ridhaa ya chama chake...Sugu anaungana na wasanii wengine toka Tanzania kama Kalama Masoud AKA Kalapina anatakayegombea Udiwani jimbo la Kinondoni-DSM kupitia chama cha CUF,na Nakaaya Sumary aliyetangaza nia ya kugombea Ubunge mkoani Arusha kwa tiketi ya CHADEMA...Hatutauza kura zetu....ila Kila la Kheri waheshimiwa watarajiwa!
na hu ndio muonekana wake na wana cha wenzake akina G-solo



wEEK MBILI MBELE KWA USAJILI WA NAMBA ZA SIMU..




SERIKALI imeongeza muda wa usajili wa simu za viganjani ili kuwezesha wananchi wengi waweze kujisajili baada ` kusikiliza kilio chao ili kuwapa fursa zaidi ya kujisajili.
Hayo yalisemwa jana Bungeni na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msollla wakati akiwasilisha hotuba yake ya makadrio ya mapato na matumizi ya fedha ya wizara hiyo. “Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu imesikia kilio cha wananchi wengi.

Imeongeza muda wa usajili wa simu za viganjani hadi Julai 15, mwaka huu baada ya hapo simu zote ambazo hazijasajiliwa zitafungwa,” alisema Profesa Msolla .
Aidha Waziri Msolla alisema jumla ya kampuni 14 hadi sasa zimepewa leseni ya kutoa huduma za mawasiliano ya simu. Aliongeza kuwa idadi ya watumiaji wa simu kwa kigezo cha njia za simu (line) zinazotumika imefikia 18,207,390, hivyo idadi hiyo ni ongezeko la asilimia 400 ikilinganishwa na watumiaji 3,542,563 waliokuwepo mwaka 2005.


Alisema idadi ya simu za mezani hadi sasa ni 174,800 ilinganishwa na 154,420 zilizokuwepo mwaka 2005. “Hii ni sawa na ongezeko la la asilimia 13.2 . ukuaji huu umepanua wigo wa mawasiliano ya simu na kuongeza huduma nyingine zinazoendana na matumizi ya simu hapa nchini Alizitaja huduma hizo kuwa ni upatikanaji wa taarifa, huduma za mtandao, ulipaji wa Ankara za simu, maji, umeme na huduma za kibenki. Awali Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilitoa agizo kuwa nambazote za simu za mkononi zisajiliwe kati ya Julai 1, mwaka 2009 hadi Desemba 31, mwaka 2009.


Awali mamlaka hiyo iliongeza muda wa mara ya pili wa miezi sita wa kusajili simu hizo, kuanzia Januari mwaka 2010 hadi Juni mwaka huu baada ule wa kwanza kuonyesha watu wengi walikuwa hawajajisajili.